Habari
MAFUNZO YA USIMAMIZI WA MAADILI YA VIONGOZI YAWAFIKIA WABUNGE
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro ikipata mafunzo kuhusu Usimamizi wa Maadili ya Viongozi wa Umma kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Mafunzo hayo yamefanyika katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma, tarehe 11 Februari, 2026.
