More Links

Webmail
PSP
FAQ

Agencies

TPSC
TGDLC

Polls

How do you rate our Website
 

In Focus

FPSS slide image

Wakazi wa Mwanza na mikoa ya jirani wakiwa katika sherehe za uzinduzi wa Wiki ya Utumishi wa Umma, uwanja wa CCM Kirumba

FPSS slide image

Bw. Dominick Minja aliyetunukiwa Nishani ya Utumishi Mrefu na Maadili Mema Daraja la pili, akiongea katika hafla iliyoandaliwa na Ofisi ya Rais-Utumishi kuwapongeza watumishi waliotunukiwa nishani

FPSS slide image

Mgeni rasmi wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Utumishi Waziri wa Fedha na Uchumi Mh. Mustafa Mkulo (wa pili kulia), akipata maelezo katika banda la Utumishi, akiwa na Kaimu Katibu Mkuu-Utumishi Bw. Eric F. Shitindi (wa kwanza kulia).

FPSS slide image

USHINDI: Watumishi wa Ofisi ya Rais wakifurahia ushindi kwa Utoaji wa Huduma Bora za Jamii, wakati wa maonesho ya Nane nane kiwanja cha Nzuguni Dodoma 

FPSS slide image

Mkuu wa sehemu ya Utumishi-Bi. Jane Kajiru akifungua mafunzo kuhusu ugonjwa wa UKIMWI kwa watumishi wa Ofisi ya Rais-Utumishi  jijini Dar es salaam

FPSS slide image

Waziri wa Nchi-Utumishi Mh. Hawa A. Ghasia (MB) akiwa katika picha ya pamoja na moja kati ya washindi wa maonesho ya Wiki ya Utumishi katika kiwanja cha CCM Kirumba, Mwanza

FPSS slide image

Kaimu Katibu MKuu, Utumishi Bw. Eric F. Shitindi (watatu kutoka kulia),  katika picha ya pamoja na watumishi wa kujitolea kutoka nchini Japani mara ya kuwapokea

FPSS slide image

Waziri wa Nchi-Utumishi Mh. Hawa A. Ghasia (MB) akihudumia wateja wakati wa maonesho ya Saba saba - Dar es salaam

FPSS slide image

Mtumishi wa Ofisi ya Rais-utumishi akieleza faida za kupima na kuwa mkweli kuhusu afya wakati wa mafunzo kuhusu ugonjwa wa UKIMWI

FPSS slide image

Kaimu Katibu Mkuu, Utumishi Bw. Eric F. Shitindi akiongea na vyombo vya habari kuhusu kauli ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) kuhusu uchaguzi mkuu

FPSS slide image

Wadau wa Ofisi ya Rais-Utumishi wakipata huduma wakati wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi, Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza

FPSS slide image

WIKI YA UTUMISHI - MWANZA: Wananchi wakipata maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na Ofisi ya Rais-Utumishi katika kiwanja cha CCM Kirumba

FPSS slide image

Watumishi kutoka katika taasisi mbalimbali za serikali wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza mafunzo kuhusu TEKNOHAMA yaliyofanyika  Morogoro

FPSS slide image

Mmoja wa watumishi wa Ofisi ya Rais-Utumishi akipata ushauri kabla ya kupima afya

FPSS slide image

Waziri wa Nchi-Utumishi Mh. Hawa A.Ghasia (MB) akimkabidhi vitendea kazi Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Bw. David K. Jairo (kushoto) baada ya kuzindua rasmi wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania

FPSS slide image

Katibu Mkuu- Utumishi Bw. George D. Yambesi, wa nne kutoka kulia waliokaa, katika picha ya pamoja na Watendaji wakuu wa Wakala wa Serikali baada ya kufungua mkutano wao wa kila mwaka

FPSS slide image

Waziri wa Nchi-Utumishi Mh. Hawa A. Ghasia (MB) akihutubia wakati wa kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, Mwanza

FPSS slide image

Kaimu Katibu Mkuu-Utumishi Bw. Eric F. Shitindi akiongea na vyombo vya habari wakati wa maonesho ya Nane nane-Dodoma

FPSS slide image

Waziri wa Nchi-Utumishi Mh. Hawa A. Ghasia (MB) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh. Abbas Kandoro tuzo wakati wa kilele cha maonesho ya Wiki ya Utumishi  baada ya mkoa wake kuibuka mshindi katika kushughulikia masuala ya ugonjwa wa UKIMWI 

FPSS slide image

Shamrashamra wakati wa kumuaga aliyekua Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi wa Umma  Bw. F.Mbaga

FPSS slide image

Waziri wa Nchi, Utumishi Mhe. Hawa A. Ghasia akisaini kitabu cha wageni wakati wa maonesho ya Nane nane-Dodoma

FPSS slide image

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mwanza wakielimishwa kuhusu matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA)  serikalini katika banda la Utumishi uwanja wa CCM Kirumba

FPSS slide image

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akimvisha Bw. Dominick A. Minja wa Ofisi ya Rais-Utumishi Nishani ya Utumishi Mrefu na Maadili Mema Daraja la pili katika uwanja wa Nyerere Dodoma

FPSS slide image

Waziri wa Nchi-Utumishi Mh. Hawa A. Ghasia akimtunuku cheti Katibu wa Baraza Kuu katika Utumishi wa Umma na Baraza la Majadiliano ya pamoja katika Utumishi wa Umma Bw. Mathias Kabunduguru baada ya kumaliza muda wa nafasi hiyo

FPSS slide image

Mteja akihudumiwa katika banda la Ofisi ya Rais, Utumishi wakati wa maonesho ya wiki ya Utumishi, uwanja wa CCM Kirumba 

FPSS slide image

Katibu Mkuu Kiongozi Bw. Phillemon Luhanjo, kati kati (waliokaa), akiwa katika picha ya pamoja na Naibu na Naibu Makatibu Watendaji walioteuliwa hivi karibuni wakati wa mafunzo elekezi kwa viongozi hao-Dodoma, Kushoto (waliosimama) ni Kaimu Katibu Mkuu-Utumishi Bw. Eric F. Shitindi

FPSS slide image

Waziri wa Fedha na Uchumi  Mh. Mustafa H. Mkulo akifungua rasmi maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, uwanja wa CCM Kirumba Mwanza

FPSS slide image

Jengo la Serikali-Mtandao lililozinduliwa sambamba na Awamu ya pili ya Programu ya Kuboresha Utumishi wa Umma.

FPSS slide image

Bw. Fredrick Mbaga, na mkewe wakiwa na  zawadi waliyokabidhiwa katika sherehe ya kumuaga Bw. F. Mbaga kwa kustaafu 

FPSS slide image

Waziri wa Nchi-Utumishi Mh. Hawa A. Ghasia akimkabidhi zawadi Katibu Mkuu-Utumishi Bw. George D. Yambesi katika hafla ya kuwapongeza watumishi waliopata nishani za utumishi wa muda mrefu

FPSS slide image

Kaimu Katibu Mkuu-Utumishi Bw. Mick Kiliba, katikati,  akiongea katika hafla ya kumuaga Bw. Fredirick Mbaga (kulia) aliyekua Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi wa Umma kwa kustaafu, kushoto, mke wa Bw. Mbaga.

FPSS slide image

Watumishi wa Ofisi ya Rais-Utumishi wakiwa na kikombe cha ushindi wakati wa maonesho ya Nane nane, kiwanja cha Nzuguni Dodoma

FPSS slide image

Bendi ikiongoza maandamano ya watumishi wa Umma kutoka taasisi mbalimbali wakati wa sherehe za uzinduzi wa Wiki ya Utumishi wa Umma  

MASWALI NA MAJIBU YA WADAU WA OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA WAKATI WA MAONESHO PDF Print E-mail

Kama sehemu ya kuelimisha kuhusu huduma zinazotolewa na serikali, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma (OR MUU) iliratibu Wiki ya Utumishi wa Umma kuanzia 16-23 Juni 2009, Pia ilishiriki maonesho ya kimataifa ya Saba Saba katika viwanja vya Mwalimu Julius K. Nyerere-Barabara ya Kilwa na Nane nane katika viwanja vya Nzuguni mkoani Dodoma 2009. yafuatayo ni maswali yaliyoulizwa na wadau mbalimbali, na majibu yake

  • Muuliza swali: Methew Modest Kirama

Swali/Maoni: Nawapongeza kwa kazi nzuri. Hata hivyo kuna mengi ya kujifunza na kufanya ili kila mara muwe na mambo tofauti ili msiwachoshe watu waliowatembelea banda hili. Hongera kwa kuleta mashine ya kuweza kuangalia kumbukumbu za zamani

Jibu: Tunashukuru kwa dhati kwa pongezi ulizozitoa. Ni kweli kuna umuhimu wa kuwa na mabadiliko ya vitu tunavyopeleka katika maonesho kila mwaka ili tusiwachoshe wateja wanaotutembelea. Aidha, tunakushukuru kwa ushauri na tunaahidi kuufanyia kazi na matokeo yataonekana katika maonyesho yanayokuja. 
  • Muuliza swali: Cecylly Cornelly Ngudungi

Tutorial Assistant – TPSC. 

Swali/Maoni: Katika kada ya utunzaji kumbukumbu tunahitaji ushirikiano wa dhati zaidi katika Idara ya Utunzaji Kumbukumbu ili kuepusha ile dhana ya watunzaji Kumbukumbu kudharauliwa, wathaminiwe na kupewa motisha ili waweze kupenda kazi zao. Utumishi simamieni kidete nyie ndio kitovu cha maendeleo katika ofisi za Serikali.

Jibu: Ofisi ya Rais, Utumishi - Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa inatambua kuwa utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka za taifa ni jambo linalohitaji michango ya wadau mbalimbali katika utekelezaji wake. Michango hiyo hutegemewa sana na Idara ili kuleta mabadiliko chanya katika fani hiyo. Hivyo, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa ipo tayari wakati wote kushirikiana na wadau mbalimbali ili kupata michango yao ambayo ni muhimu katika kuboresha utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka.

Baadhi ya maeneo ambayo Idara imeshashirikiana na wadau ni pamoja na kuanzishwa kwa kada ya Watunza Kumbukumbu, kuanzishwa kwa mafunzo ya Cheti na Diploma katika chuo cha Utumishi wa Umma, maandalizi ya miongozo na taratibu mbalimbali za utunzaji kumbukumbu na nyaraka kama vile Sheria na Kanuni za utunzaji kumbukumbu na nyaraka.  Baada ya kuanzisha Kada ya utunzaji kumbukumbu na nyaraka za Taifa, na kuanzishwa kwa mafunzo ya cheti na Diploma katika Chuo cha Utumishi wa Umma, Idara imekuwa ikihamasisha wakuu wa ofisi za Umma na watendaji wengine ili waweze kutambua umuhimu wa fani ya utunzaji wa kumbukumbu , hivyo kuweza kuipa thamani inayostahili. Hivi sasa suala la utunzaji wa kumbukumbu linazungumzwa katika ngazi mbalimbali za utendaji. Aidha watunza kumbukumbu na nyaraka hupelekwa mafunzo ya Cheti, Diploma pamoja na semina za utunzaji kumbukumbu. Pia watumishi hao hupandishwa vyeo baada ya kupata sifa zinazotakiwa.  

  • Muuliza Swali: Happy Daniel Onim

 Swali/Maoni Tungependa kila mwisho wa mhula wa mafunzo (semester) wanafunzi tupelekwe National Archive kwa Mafunzo zaidi na tujue jinsi ya kutunza kumbukumbu katika Nyaraka za Taifa.   

 

Jibu: Ofisi ya Rais, Utumishi - Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa inawakaribisha wakati wowote wanafunzi wanaohitaji kujifunza zaidi kuhusu namna bora ya kuhifadhi Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa.  Jambo la msingi linalotakiwa kufanyika ni kutoa taarifa mapema ili maandalizi yaweze kufanyika.  Aidha baadhi ya Taasisi za elimu huomba na kuleta wanafunzi kwa ajili ya mafunzo hayo.     

 

  • Muuliza swali: Tito David Ntanga

            S.L.P 76161 Simu. 0784856244 

Swali/ maoni: Kwa kuwa kuna habari nyingi zimeingizwa kwenye mtandao kwa hali hiyo mishahara/matokeo ya mitihani vyote hivyo tunavipata kwenye mtandao, sasa tunaomba kuwa habari zinazohusu watu wenye ulemavu wa aina zote ziwekwe kwenye mtandao ili jamii iweze kuwaelewa jamii ya watu wenye ulemavu kupitia mitandao hiyo. Ofisi ya Rais - Utumishi kupitia Kitengo cha Anuai za Jamii inachukua hatua mbalimbali kushughulikia watu wenye ulemavu ambao ni watumishi wa umma. Hatua hizi ni pamoja na kuandaa Mwongozo kuboresha mazingira ya kazi kwa watumishi wenye ulemavu katika utumishi wa umma. 

Jibu: Taarifa mbalimbali zinazohusu watumishi, wakiwemo watumishi wa umma wenye ulemavu zimewekwa katika tovuti ya Ofisi ya Rais-Utumishi. Taarifa hizo ni pamoja Mwongozo wa Huduma kwa Watumishi wa Umma wenye ulemavu, Watumishi waliopatiwa ufadhili wa Shahada ya pili kwa mwaka 2008-2009 wakiwemo watumishi wenye ulemavu, tangazo kuhusu ufadhili wa Shahada ya pili kwa watumishi wanawake na watumishi wenye ulemavu na taarifa ya utekelezaji wa Mwongozo kuhusu huduma wanazotoa waajiri katika sehemu za kazi kwa watumishi wenye ulemavu. Ofisi ya Rais-Utumishi itaendelea kutoa taarifa mbalimbali kupitia tovuti, maonesho ya Saba Saba, maonesho ya Nane Nane, vipindi vya Radio na Luninga, pamoja na magazeti ili taarifa ziweze kuyafikia makundi yenye ulemavu. 

  • Muuliza Swali: Yahya Mohamed Said

             Simu: 0784505727/ 0715 505727 

Swali/Maoni: kuna matumizi mabaya ya madaraka katika taasisi za Afya na Polisi. Jibu: Ofisi ya Rais-Utumishi imeanzisha mfumo wa malalamiko katika taasisi za umma kwa lengo la kuboresha huduma. Hivyo wananchi wanashauriwa kutumia mfumo wa malalamiko kuwasilisha kero/malalamiko yao. Mfumo huu tayari unatekelezwa Wizara ya Afya, Wizara ya Mambo ya Ndani, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Ofisi ya Rais-Utumishi, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Manispaa ya Ilala na Hospitali ya Amana. Mpango uliopo ni kwa mfumo huu kuwepo katika taasisi zote za umma. Hata hivyo, pale ambapo hakuna mfumo, kero zinaweza kuwasilishwa kwa Mkuu wa taasisi husika kwa kutumia barua, barua pepe, nukushi au kupitia vyombo vya habari na tovuti ya wananchi yenye anuani;  www.wananchi.go.tz 

  • Muuliza swali: Henry Rabi Savi

                      Simu:  0717583435

 Swali/ maoni: Maadili kwa watumishi wa umma bado hayaridhishi japo kanuni za maadili kwa watumishi wa umma, (watumishi wanavujisha siri za Serikali, mavazi yasiyo rasmi, upendeleo kwenye kutoa huduma). Tuna shauri ofisi za maadili zifunguliwe katika ngazi ya Wilaya na Mkoa Jibu: kwa mujibu wa sheria namba 8, ya utumishi wa umma ya mwaka 2002, kifungu cha 35 sehemu ya 2 (a) waajiri wamepewa mamlaka ya kushughulikia masuala yote ya maadili na nidhamu kwa watumishi. Hivyo jukumu la kusimamia maadili kwa watumishi wa umma linapaswa kushughulikiwa na kila mwajiri. Hivyo endapo kuna masuala ya ukiukwaji wa maadili kwa watumishi waajiri katika ngazi ya wilaya wanapaswa kushughulikia.  

  •  Muuliza swali: Hamis Rupia

                      S.L.P 169,      

                        Songea.

 Swali/ maoni: Wananchi mikoani hawajui ni vipi watatoa malalamiko yao pindi kunapopatikana matatizo.

Jibu: Ofisi ya Rais-Utumishi imeanzisha mfumo wa kushughulikia malalamiko ambao tayari unafanya kazi katika taasisi saba za umma. Mpango wa utekelezaji uliopo kwa sasa ni kueneza mfumo huu katika taasisi zote za umma. Hata hivyo, pale ambapo hakuna mfumo, kero zinaweza kuwasilishwa kwa Mkuu wa taasisi husika kwa kutumia barua, barua pepe, nukushi au kupitia vyombo vya habari na tovuti ya wananchi yenye anuani;  www.wananchi.go.tz   

Swali/ Maoni: Kwanza kabisa napenda kushukuru kwa Katibu Mkuu  na Watumishi wote wa Umma. Napendekeza  Mtumishi yeyote anapomaliza makato yake kama vile NSSF kwenda masharti ya kudumu anaposubiri mpaka kustaafu pesa haiwezi kumsaidia/ kusomesha au kujikimu (thamani inakuwa imesisha).

  •          Muuliza swali: Raymond Lugemalila Mwombeki

                        Simu No. 0756625737

Jibu: Nia ya Serikali kuanzisha Mifuko ya Mafao ya Pensheni na Hifadhi za Jamii ni kuwawezesha watumishi wake, waweze kupata mafao mazuri yatakayowawezesha kumudu maisha yao kwa urahisi pindi wanapostaafu au kukoma utumishi wao. Kwa mujibu wa Sheria ya NSSF Cap. 50 R.E. 2002 Sehemu ya 5 inayohusu Mafao ya Watumishi wanaochangia NSSF, na  kwa mujibu wa Vifungu 21, 22, 23, vya Sheria hiyo ili mtumishi aweze kulipwa mafao lazima awe ametimiza miaka 55 au 60. Hivyo basi kwa kuzingatia sheria hiyo Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii unao utaratibu wa kuhifadhi mafao ya watumishi wanaobadilisha masharti ya kazi kutoka “Operational Service” kwenda “Permanent and Pensionable” mpaka hapo mtumishi atakapofikisha umri wa kustaafu. Aidha, mafao hayo hulipwa pamoja na “bonus” ili kuepuka  ‘devaluation’ ya fedha zilizoifadhiwa kwa muda mrefu. 

Last Updated ( Tuesday, 27 October 2009 )
 
< Prev   Next >

Events Calendar

September 2010 October 2010
Su Mo Tu We Th Fr Sa
Week 35 1 2 3 4
Week 36 5 6 7 8 9 10 11
Week 37 12 13 14 15 16 17 18
Week 38 19 20 21 22 23 24 25
Week 39 26 27 28 29 30

Upcoming Events

There are no upcoming events currently scheduled.

Who's Online

We have 15 guests online